Saturday, June 6, 2020

Tafakari. Sherehe ya Utatu Mtakatifu

Somo la Kwanza. Kut. 34: 4b-6, 8-9

Somo la Pili. 2 kor. 13:11-14

Injili. Yn 3: 16-18

Je, tunaelewa nini kuhusu utatu Mtakatifu wa Mungu? Zamani za kale katika kijiji kimoja nchini Nigeria mzungu mmishionari alifika na kwanza kufundisha wenyeji kuhusu Ukristu. Kwanza alitaka kuanza kufundisha kuhusu utatu Mtakatifu. Alianza kwa kusema ya kwamba kuna Mungu mmoja tu. Halafu akafundisha kuwa kuna mwana wa Mungu na jina lake ni Yesu. Mzee mmoja akamuliza mmishionari, ulituambia ya kwamba kuna Mungu mmoja tu, na sasa unaongea kuhusu mwana wake. Hii inamaanisha Mungu ana mke basi. Watu wakamuunga mkono mzee yule. Mmishionari akajibu, sijasema kuwa Mungu ana mke. Makalio yako ndiyo yamesema kuwa Mungu alikuwa na Mwana, kwa hiyo kama alikuwa na mwana ni lazima alikuwa na mkee pia. Akasema huyo mzee. Mmishionari akampuuza mzee yule na kuendelea na mafundisho yake kuhusu utatu Mtakatifu. Mwishowe yule mzee akamuona mmishionari kuwa ni mwendawazimu. Alimpuuzia yule mmishionari na kuamua kwenda kunywa pombe ya mnazi. Deturi ya kikristo inamwonesha Mungu katika utatu; Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Utatu huu ni Mgumu sana kuelezea kwa wakristo.

Katika mafundisho ya katekisimu tunaulizwa kila mara, Mungu ana nafsi ngapi? Huwa tunajibu kwamba, kuna Mungu Babu, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu. Na katekista akituuliza, Je? Kuna Mungu watatu? Tunajibu-La, kuna nafsi tatu katika Munug Mmoja. Tunaporudi jibu namna hii tunapandishwa viwango na kuwa waumini wa kanisa. Ni sawa na kusema moja kuongeza moja, na kuongeza moja ni sawa na moja. Fundisho la Kiroho siyo somo la hesabu. Tunapaswa kujiuuliza mafundisho kuhusu utatu Mtakatifu yanatuambia nini juu ya uhusiano wetu na Mungu? Tunaelewa nii juu ya uhusiano huu? Kuna maandiko mengi na ishara katika agano jipya ambayo yanaongea juu ya Utatu Mtakatifu. Maandiko haya na kanuni hizi zilitumiwa na mababu zetu wa Imani katika desturi Fulani. Lakini kuna maswali ya kutafakari katika mazingira yetu ya kiafrika. Kama mtanzania, ninelewa nini juu ya Utatu Mtakatifu wa Mungu? Kuna chochote katika misingi ya kiafrika kinachoweza kutuonehsa na kutufundisha kuhusu Utatu Mtakatifu wa Mungu. Kuna viashiria mbalimbali vinavyoweza kutudhihirishia utatu Mtakatifu wa Mungu. Pia ni Muhimu kutambua hizo ishara. La shivyo tutabakia kama huyo mzee wa Nigeria hatuwezi kuuelewa Utatu Mtakatifu wa Mungu.
Katika vijiji vyetu, ninauhakika umewahi kumwona mwanamke aliyebeba chungu kichwani mwake na mtoto amefungwa mgongoni akielekea nyumbani kutayarisha chakula kwa familia yake na labda ni mjamzito. Taswira hii ya mama wa kiafrika inatupatia njia ya kuelewa kuhusu Utatu Mtakatifu. Picha ya mama anayebeba maji, mtoto mgongoni n mwingine tumboni inatupatia picha ya Mungu anayejengwa sehemu nyingi, nafsi nyingi, uhalisia mwingi, na ubora mwingi kwa wakati umoja akiwa Mungu Mmoja. Mungu wetu kama mama wa kiafrika  anaunganisha  sehemu nyingi mungu wetu ni Mungu Mama, Mungu Baba, Mungu mwana, binti, kaka, dada na wakati huo huo ni Mungu yule yule. Hii ndiyo njia rahisi mojawapo tunayoweza kuitumia kueleza juu ya Mungu wa Utatu katika desturi za kiafrika.
Utatu Mtakatifu ni kama ishara kwetu tumekombolewa na Mungu kupitia Yesu Kristo, mwana wake wa pekee kwetu kwa kufa na kufufuka kwake. Tunakumbushwa kwamba tunaokolewa na Mungu kupitia kwa Yesu Kristu katika nguvu za Roho Mtkatifu. Kwetu sisi wa Kristu Utatu Mtakatifu ni njia yetu ya pekee kumweleza Mungu na kile alichotufanyia na anachoendelea kutufanya katika maisha yetu. Mungu anafunuliwa kwetu kwa njia ya Kristu na ndani ya Kristu. Tunajua Mungu kama Baba, Mwana na Roho kwa sababu Yesu alikuja kutuokoa kwa msaada wa Roho Mtakatifu na anatuonyesha njia ya kuelekea kwa Mungu.
Hivyo katika sikukuu ya leo tunajifunza nini? Tunakumbushwa kuomba ishara ya msalaba tukiwa na maana na heshima kubw. Inaunganisha fumbo la utatu Mtakatifu na ishara ya ukombozi wetu kwa kuteswa kwa Yesu, kifo na ufufuko wa Yesu. Tufanye ishara ya msalaba kwa heshima na hadhi kuu na kwa myo wa sala ya kweli. Tunahitaji kuona utatu kama mfano mwema kwa familia zetu za Kikristu. Tumeumbwa kwa upendo tuwe jumuia ya watu wenye upendo, kama vile Baba, Mwana na Roho wameungana katika upendo. Umoja na furaha katika uhusiano wa Baba, Mwana, na Roho ndiyo mfano mwema kwetu katika uhusiano wa familia za wakristu. Familia zetu zinakuwa za Kikristu tunapoishi katika uhusiano wa upendo na Mungu na watu wengine.
Tunaalikwa tuwe bora kama Mungu wa Utatu Mtakatifu katika uhusiano wetu wote. Jamii  za kisasa wanafuata mtindo wa mimi ni mimi, wa kibinafsi. Lakini mafundisho ya Utatu Mtakatifu uatupatia hamasa ya kuiga mtindo wa umoja, “Mimi na Mungu na Jirani.” Nitakuwa mkristo iwapo ninafuata upendo wa Mungu kwa watu wote. Kama wana wa Mungu tunaalikwa kujenga maisha ya upendo katika familia zetu, kanisa, jumuiya na nchi. Kama Mungu mwana tunaalikwa kuwa wapatanishi, kutengeneza Amani. Kama Mungu, katika Roho Mtakatifu ni jukumu letu kujifunua na kufundisha kweli ili kuondoa giza la kiroho. Utatu Mtakatifu atuletee upendo, Amani na umoja katika Roho zetu, familia, kanisa na katika nchi yetu ya Tanzania.











No comments:

Post a Comment

Sermon for 17th Sunday in Ordinary time, Year A.

Sermon for 17th Sunday Ordinary time, year A. Gospel. Mt. 13: 44-52 In the Gospel of today, we are presented with three ...