Saturday, April 18, 2020

Dominika ya 2 ya Pasaka, Aprili 19, 2020, Mwaka A


Dominika ya 2 ya Pasaka, Aprili 19, 2020, Mwaka A 


Injili: Yn 20: 19-31






Injili ya leo inatueleza ambacho Yesu Kristo alifanya baada ya kufufuka Kwake. Wanafunzi wake walikuwa wamekusanyika katika chumba kidogo. Walikuwa bado wakiogopa Wayahudi kwamba Wayahudi watawaua kwa kuwa walikuwa wafuasi wa Yesu Kristo. Kwa ghafla bila kutegemea kabisa, Yesu aliwatokeza mbele yao. aliwaonyesha mikono yake na pande zake zilizotobolewa na misumari.  Aliwapa ujumbe wa amani na aliwaahidi kwamba amani Yake haiwezi kuondolewa kutoka kwao. uwepo wa Yesu ilikuwa ishara ya amani.

Wakati Yesu alipowatokeza wanafunzi wake kwa mara ya kwanza, ni kumi tu waliokuwepo. Tunaambiwa kuwa, kwa sababu fulani, mmoja wa wanafunzi, Tomaso, hakuwepo kwenye hafla hii. Hatujui kwanini hakuwepo. Kilicho muhimu ni kukutana kwake na Yesu Aliyefufuka. Alikataa kuamini kuwa Bwana amefufuliwa kutoka kwa wafu na alikuwepo kati ya wafuasi wake. Alitaka kuona kwa macho yake mwenyewe na alitaka kugusa mwili wake. Tomaso binafsi alitaka kukutana na Yesu ili kuamini ufufuo wake. Je! Kwanini Tomasi hakuamini juu ya ufufuko wa Yesu Kristo? Walipomwambia kwamba Yesu amefufuka na ameonekana kwao labda alishangaa na akajiuliza basi kwanini bado mnajificha? Alihisi kama wangemwona Yesu kweli wangekuwa wakipiga kelele kwa sauti ya juu wakiuambia ulimwengu kuwa Yesu yu hai. Kwa kuwa wamejificha na walikuwa bado wanaogopa Wayahudi, hakuweza kuamini amefufuka. Kwa kweli Tomaso alikuwa mtu wa imani. Katika maisha yake alifanya hivyo tu. Alienda mbali sana India na akafa kwa imani yake.

Kama tunavyojifunza katika Injili, Yesu alionekana wiki moja baadaye siku ya Jumapili, na alikutana nao kwa mara nyingine akawatakia Amani. Kisha akamwita Tomaso akamkemea kwa kutokuamini kwake, akamwamuru amshikeshike na kupapas mikono yake ili aamini. Je! Alimgusa Yesu Kristo? Maandiko yanatuambia kuwa macho ya Thomaso yalifunguliwa na kutamka kwa Imani. "Bwana wangu na Mungu wangu!" Wakati huo, lazima Tomaso alistaajabu na kushangaa. Mwisho wa tukio hili, Yesu alimpongoza Tomaso kwa imani yake kwake mara tu alipokutana naye. Yesu aliwahimiza wanafunzi wake kuaminipasipo kuona. Imani kwa kweli ni kukutana na Mungu kwa jicho la ndani la kiroho na kumtegemea. Na kweli tangu sasa, ufuasi wa Yesu ni kumwamini pasipo kumwona, lakini ni kutunza ushuhudo kuwa Yesu yu hai, kwamba yeye yuko pamoja nao katika yote wanayofanya, kwamba yeye ndiye chanzo cha amani yao na furaha katika majaribu yao yote na dhiki.

Je! Tunaweza kujifunza nini katika kwa Injili ya leo? Kwanza, hofu ni kinyume cha imani katika Mungu. kama wanafunzi tunaweza kuwa na woga mwingi. Hofu ya kupoteza kazi, woga wa kupoteza utajiri wetu, woga wa kupoteza maisha, hofu ya hatma yetu. Lakini sikukuu ya ufufuo inatuambia kwamba Yesu Kristo ametukomboa katika woga wetu na wasiwasi. Tunachohitajika kufanya ni kumwamini kila wakati. Kwa kumwamini Yesu Kristo tutashinda woga wetu. Kuogopa kitu chochote hututenganisha na Mungu. Pili, ni vizuri kujiuliza kuhusu uwepo wa Mungu katika maisha yetu. Tomaso alitafakari kufufuka kwa Yesu Kristo. Lakini bado alikuwa tayari kujifunza zaidi juu ya Yesu Kristo. Hata alienda India kuhubiri neno la Mungu. Ni vizuri kutafakari uwepo wa Mungu katika maisha yetu haswa tunapopitia magumu katika maisha yetu. Lakini tunatakiwa kuwa tayari kama Tomaso ili tufundishwe na  Yesu Kristo. Tafakari zetu juu ya uwepo wa Mungu unaweza hata kuimarisha imani yetu. Tunahitaji kumruhusu Yesu Kristo aongoze maisha yetu. Tunahitaji kutoa maisha yetu kwa Yesu Kristo na kwa mara nyingine tutahisi uwepo wa Mungu katika maisha yetu. Matatizo na shida zetu katika maisha yetu ziko ili kutuimarisha, na kuimarisha imani yetu kwa Yesu Kristo.
         Mtu mmoja alikuwa na shida nyingi maishani mwake. Kwa hivyo aliomba Mungu aingilie kati katika maisha yake na atatue shida zote. Aliomba mchana na usiku na siku moja akasikia sauti kutoka juu ikisema: "Nataka uende kusukuma jiwe hilo kubwa.” Mtu huyo aliamka na akiwa na shauku. Alikimbia kutafuta lile jiwe na kuanza kulisukuma. Alisukuma na kusukuma, lakini hakuambulia chochote. Aliendelea kusukuma mwamba  huo kwa siku nzima. Siku iliyofuata alifanya vivyo hivyo, lakini jiwe halikuhama hata kidogo. Kwa miezi mitatu mtu huyo aliendelea kusukuma mwamba mkubwa. Mwishowe alichoka na akaacha kusukuma. Usiku huo aliota ndoto nyingine, na akasikia sauti ikisema: "Kwa nini umeacha kusukuma jiwe?" "Hakuna kilichobadilika katika maisha yangu, bado kuna shida na jiwe bado liko pale pale," - akajibu mtu huyo. "Hakuna kilichotokea? Jitazame mwenyewe! Umekuwa mtu imara na mwenye kujitambua Zaidi.  Umekuwa shupavu Zaidi. Wewe ni mtu aliyebadilishwa sasa! Kusukuma kumekubadilisha! Hata hivyo, sikukuambia uliondoe jiwe. Nilikuambia usukume tu. Wakati utakapofika, nitaliondoa mwenyewe! "Kama unavyoona, wakati mwingine magumu katika maisha yako yapo ili kukufanya uwe imara na kukubadilisha. Matatio hayapo ili uyaondoe wewe nao. Wakati ukifika, Mungu wetu atatuokoa kutoka katika shida zetu.

No comments:

Post a Comment

Sermon for 17th Sunday in Ordinary time, Year A.

Sermon for 17th Sunday Ordinary time, year A. Gospel. Mt. 13: 44-52 In the Gospel of today, we are presented with three ...